Uchunguzi
 

Maandishi Matupu

Karibu Kwenye Idhaa Ya KiSwahili Ya Sauti Ya Nijeria.......................

Leo tarehe 19 March ni sikukuu ya EID-EL-MAOLUD, sikuu ambayo waislamu wenye imani duniani kote washerekeya kuzaliwa kwa nabii Mouhammad. 

Sherehe hii ni sikukuu ambayo waislamu wenye imani husoma mchana hadi usiku kitabau cha Korani takatifu, vitabu vya mfano wa maisha ya nabii Muhammad na vitabu vingine vya kukuza imani ya kiislamu,sherehe hii hutukia kila tarehe 12 ya mwezi wa Rabiul Awwal, mwezi wa tatu wa kalenda ya kiisalamu.

Serekali ya nigeria imetangaza siku ya leo kuwa siku ya mapumziko nchini kote.

Imam Fuad-adeyemi wa muskiti iitwayo Al habibiyah huko jijini Abuja mji mkuu wa Nigeria alieleza kwa vyombo vya habari umuhimu wa kusherekeya sikukuu ya leo , wanafunzi kadhaawa ma darasa za elimu ya kiislamu walihotubia pia kuhusu sikuu ya leo na umuhimu wake. 

Eid-el-maulud inasherekewa Nigeria kwa njia za michezo kadhaa ,ikiwemo  kutembea juu ya farasi na kubadilisha zawadi baina waamini wengi wa kiislamu nchini kote nigeria.

Ofisi ya huduma za raiya nchini Nigeria inayo julikana tena kwa jina la DUE PROCESS imesema kwamba wa kontrakta waliopewa projeti ya kukuza uduma za umeme nchini kote, itabidi irudishe kwa serekali billioni 3.3 waliodai kutumia kwa kukuza huduma hizo

Kiongozi wa ofisi hio Bwana EMEKA EZE, alishuhudia mbele ya tume la wakilishi kwa huduma za moto wa umeme kwamba ofisi yake iliomba fedha karibu billioni 150.6 za Naira, ila ofisi yake haikuelezwa wakati malipo yale yalifanyika.

Bwana Eze amesema tena kwamba hatua hio yakusikilizwa mbele ya tume la bunge la taifa ni hatua muhimu sana , ikieleza kwamba maafisa wote wasio julikana na raiya ya walio pokonya mali ya taifa, faili zao zitafunuliwa mbele ya tume hilo kwa muda wa siku 60.

Wa seneti nchini Nigeria wametangaza kuweka malipizi kali kwa watu wanao husika, kwa kupotea angani kwa ndege la BEECHCRAFT, wakiwapa ma saa 48 kwakuleta ripoti kama ndege hio imekwenda wapi. 

Msimamizi wa kamati ya seneti kwa huduma za safari ya anga, Chief Anyim –Udeh aliye tangaza hayo alipokuwa akitoa ripoti kwa wa seneti kuhusu kupotea kwa ndege hio hapo jijini Abuja. 

Chief Udeh ameeleza tena kuwa mambo yote sio barabara kabisa katika sekta ya safari angani na akisema kuwa hatua uhimu zimechukuliwa sasa  kwa kutatua  maswala yale. 

Mwandishi wetu Obiora Ani, ameripoti kwamba seneti  imehakikisha uteuzi wa watu 27 na msimamizi mpya wa tume lile.

 
 

Home | Contact | VON | Contact Us | archive
Webmaster@voiceofnigeria.org :Change Password :VON Staff Sign Up
Copyright© 2007. All Rights Reserved Voice Of Nigeria. Developed by: VON ON-LINE

7255KHz 41m; 9690KHz 31m; 11770KHz 25m; 15120KHz  19m