COMORO
Kisiwa cha Anjouan kimetekwa masaa ma chache
kiisha jeshi la Muungano wa Africa kuwasili kwakuunga mkono
majeshi ya serekali kwaku mutimua coloneli muasi Mohamed Bacar
aliye chukua madaraka kisiwani humo mwezi wa Mei.
Kuchaguliwa kwake kama rais wa kisiwa cha anjouan
mwaka jana kulitangazwa kama ni kinyume cha sheria ya serekali
ya Comoro pamoja Umoja wa Afrika.
Msemaji wa jeshi la Comoro Meja Ahmed Sidi
akizugmuza kutoka kisiwa cha Moheli kilichon jirani na kile cha
Anjouane, amesema kisiwa hicho hadi sasa kinakabidhiwa na jeshi
la serekali. Ameongeza nakusema kuwa hadi sasa hakuna jeshi wa
serekali ama ule wa Muungano wa Afrika aliye uwaua ama
kujehuriwa,
Na alihakikisha kwamba viongozi wa waasi wale
walikimbia na hakuna aliyekamatwa hadi sasa.
Awali maafisa wa Comoro walisema kundi la kwanza
la wanajeshi 450 la Muungano wa Afrika liliingia usiku wakuamkia
leo kutokea baharini na baadaye kidogo walifanikiwa na kuteka
uwanja wa ndege wa Ouani na baadaye wakauteka mji wa Mustamudu.
Milio ya bunduki na makombora mazito yalisikika
wakati wanajeshi hao walipokua wakiingia mapema Alfajiri ya Juma
nne.
Wanajeshi wa Comoro wanasaidiwa na jeshi la
Muungano wa Africa wanaofikia 1500 wakijimuisha wote kutoka
Tanzania, Senegal na Sudan.
Makamu rais wa serekali kuu amesema kwamba
kiongozi huyo muasi atakamatwa nakupelekwa mahakamani kwa kujibu
mashtaka ya uhalifu wa kivita.
MISRI
Maafifa wa usalama nchini Misri wametangaza
kwamba mashua ya kivita ya Marekani imefungulia risasi boti ya
wenyeji katika mfereji wa Suezi, nakusababisha kifo cha mtu
mmoja wa wengine wawili kujeruhiwa vikali.
Kikosi cha Marekani kimekusudia kufungua risasi
kwa boti hio kiisha kuwaamuru wasi ijogeleye meli yao.
Meli hio ilikuwa na biashara ikiuza kwa meli
zinazopita katika mfereji wa Suezi, ambako ni njia pia ya jeshi
la Marekani.
Meli hio ya kikosi cha Marekani ipo hapo
ikitarajia kupewa ruhusa kupita bahari ya Mediteranea.
MUSUMBIJI
Musumbiji na Ureno umeweka saini mkataba ya
urafiki na usafiri, na nchi hizo zimerudia tena mkataba wao wa
mwaka wa 1991 kwa kuondolea malipo kadhaa kwa raiya wao watapo
safari katika chi hizo mbili.
Hii ni hatua ya kwanza kwa Ureno kuanza uasiliano
wa kiuchumi na nchi hio ya ukoloni wake zamani, Rais Anibal
Cavaco Silva yuko wizarani Musumbiji kwa muda wa siku tatu toka
alipo wasili siku ya jumatatu kwa kukaza urafiki wa kiuchumi na
wingine.
Moja ya mkataba walio saini ni matumizi ya
liseni yakuendeza gari moja kwa nchi hizo mbili,ingawa pia
majeshi ya Ureno yataleta mazoezi kwa wenzio wa Musumbiji.
Nchi ya Musumbiji ilijipatia uhuru toka ukoloni
wa Ureno mwakani 1975.